IQNA

Viongozi wa Kikristo wa Marekani wataka kuzuiwa dharau dhidi ya matukufu ya Kiislamu

12:11 - April 10, 2011
Habari ID: 2103258
Viongozi wa baadhi ya makanisa ya Marekani wametoa taarifa ya pamoja wakilaani kitendo cha kukosewa heshima Qur'ani Tukufu katika jimbo la Florida nchini humo na kutaka kudumishwa mavumiliano miongoni mwa wafuasi wa dini tofauti nchini.
Wamesema kitendo cha Terry Jones cha kuchoma moto Qur'ani Tukufu kimewadhuru wafuasi wa dini zote ulimwenguni. Wamesema kuwa kitendo hicho si tu kwamba kimewadhuru Waislamu wa Marekani na sehemu nyingine za dunia bali kinakinzana na thamani za kiutu na mafundisho ya Kikristo. Wametaka serikali ichukue hatua za lazima kwa ajili ya kukabiliana na vitendo kama hivyo vinavyokwenda kinyume na misingi ya kidini na kisheria nchini. Viongozi hao wa kidini wamesema kuwa wanapinga kila aina ya chuki, ubaguzi na utumiaji nguvu dhidi ya Waislamu kwa kisingizio cha uhuru wa kusema. 771140
captcha