Akizungumza kwa njia ya simu na Spika wa Bunge la Lebanon Nabih Beri, Rais Ahmadinejad amesema kuwa njama za maadui dhidi ya Iran na Lebanon zimefeli kutokana na nchi mbili hizi kushirikiana kwa karibu na kuzungumza kwa sauti moja. Amesifia mitazamo sawa ya nchi hizo mbili katika masuala ya kieneo na kimataifa na kusema Lebanon imedhihirisha uadilifu wakati wote inapojadili masuala ya kieneo na kimataifa. Spika wa Bunge la Lebanon Nabih Beri kwa upande wake ameipongeza Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa kuwa kinara wa kutetea haki za walio wengi na vile vile kuwa kipaza sauti wa nchi zilizofinywa na kubanwa na Wamagharibi.
775339