IQNA

Mkakati wa kukabiliana na wanaoivunjia heshima Qurani Tukufu

14:07 - April 19, 2011
Habari ID: 2108463
Wakuu wa vyama kadhaa vya kisiasa nchini Pakistan, viongozi, wa kidini na maafisa waliostaafu jeshini wanakutana Aprili 21 kwa lengo la kujadili vitendo vya kuvunjiwa heshima Qurani Tukufu katika nchi za Magharibi na kutafuta njia ya kusitisha vitendo hivyo.
Kikao hicho kimeandaliwa na chama cha Tehrik-i-Hurmat-i-Quran na kati ya walioalikwa kuhudhuria kikao hicho ni Syed Munawar Hasan, Maulana Fazlur Rehman, Hafiz Muhammad Saeed, Maulana Samiul Haq, Sahibzada Abulkhair Zubair, Professor Sajid Mir, Raja Zafarul Haq, Chaudhry Shujaat Husain na Jenerali Mstaafu Hamid Gul.
Katika miezi ya hivi karibuni kumeshuhuydiwa ongezeko kubwa la vitendo vya kuvunjiwa heshima Qurani Tukufu katika nchi za Magharibi hasa Marekani.
777035
captcha