Hayo yamesema na Bi. Rima Fakhri, mwanachama wa Baraza la Kisiasa la harakati ya Hizbullah ya Lebanon katika mazungumzo yake na IQNA. Ameashiria vitendo vya kubakwa wanawake na kuvunjiwa heshima Qur'ani nchini Bahrain na akaongeza kuwa mambo hayo hayawezi kukubaliwa na yanalaaniwa na wanaharakati wote wa kutetea haki za binadamu.
Mwanafikra huyo wa Kiislamu amesisitiza kuwa ni wajibu kwa Waislamu wote kuwatetea watu wanaodhulumiwa na kukandamizwa na kuongeza kuwa uhalifu na jinai za kutisha zinazofanywa na utawala wa Aal Khalifa nchini Bahrain unagusa na kuumiza hisia za kila mtu huru hususan Waarabu na Waislamu.
Amesema Waislamu wote wanawajibika kushikamana na kuunda nguvu moja ya mashinikizo dhidi ya utawala fasidi na wa kidikteta wa Aal Khalifa huko Bahrain na vilevile jumuiya zinazoshirikiana na utawala huo dhidi ya wananchi ambao dhambi yao kubwa ni kudai haki zao za kisheria na kibinadamu. 786275