IQNA

Kongamano la Kimataifa la Muungano Dhidi ya Ugaidi kwa Ajili ya Amani Adilifu lafanyika Tehran

10:41 - May 15, 2011
Habari ID: 2121770
Kongamano la Kimataifa la Muungano Dhidi ya Ugaidi kwa Ajili ya Amani na Udilifu linafanyika Tehran limenaza jana Mei 14 mjini Tehran. Zaidi ya wasomi 150 kutoka nchi mbalimbali duniani wanajiunga na wenzao Wairani kujadili masuala ya amani na mbinu za kukabiliana na ugaidi.
Kongamano hilo linakusudia kuimarisha maelewano, hekima, na juhudi zenye kufuata uadilifu katika uga wa kimataifa katika kukabiliana na ugaidi.
Katika kongamano hilo kutakuwa na vikao vya kijadili maana ya ugaidi, misingi ya ugaidi, magaidi, uharibifu unaosababishwa na ugaidi na njia ya uadilifu ya kukabiliana na ugaidi.
Pembizoni mwa kikao hicho kutakuwa na maonyesho ya Wairani walioathiriwa na ugaidi.
Washiriki wa kongamano hilo la siku mbili pia watatembelea haram takatifu ya Imam Khomeini RA , muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
790906
captcha