Kongamano hilo litajumuisha wajumbe 800 kutoka nchi 12.
Lengo la kongamano hilo limetajwa kuwa ni kubuni mpango wa kukabiliana na umasikini katika kiwango cha kitaifa na kimataifa.
Wajumbe kutoka nchi kama vile Malaysia, Yemen, Afghanistan, Indonesia na Mauritius watahudhuria kikao hicho. Mada zitakazojadiliwa kuhusu Taasisi Ndogo za Fedha za Kiislamu ni kama vile mbinu za kupunguza umasikini, Zakat, Waqfu, mbinu za kisasa katika uendesha Taasisi Ndogo za Fedha za Kiislamu, matumizi ya teknolojia ya kisasa na Taasisi Ndogo za Fedha za Kiislamu katika jamii zisizokuwa za Waislamu.
795314