IQNA

Nchi za Kiarabu zalaani jinai za Israel dhidi ya Wapalestina na Wasyria

14:56 - June 08, 2011
Habari ID: 2134945
Jumuiya ya Nchi za Kiarabu imelaani vikali jinai ya utawala haramu wa Israel dhidi ya raia wa Syria na wakimbizi wa Palestina huko Lebanon na Syria.
Vikosi vya utawala wa Kizayuni wa Israel viliwaua shahidi raia 28 na kuwajeruhi wengine 350 hivi karibuni wakati wa kumbukumbu ya mwaka wa 44 tokea Wazayuni wateke ardhi zaidi za Waarabu. Siku hiyo hujulikana kama Siku ya Naksa au Siku ya kushindwa.
Utawala Wa Kizayuni umekuwa ukitelekeza jinai na mauaji ya umati dhidi ya Wapalestina kwa miaka 63. Katika kipindi hicho Wazayuni wamewapkonya Wapalestina haki zao ikiwa ni pamoja na kupora ardhi zao, imesema taarifa ya Umoja wa Nchi za Kiarabu.
Utawala wa Kizayuni umekaidi amri ya Umoja wa Mataifa ya kuondoka katika ardhi za Wapalestina unaozikalia kwa mabavu.
805129
captcha