IQNA

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Nchi za Kiislamu kukutana Kazakhstan

14:49 - June 22, 2011
Habari ID: 2142260
Ajenda iliyojaa inawasubiri mawaziri wa mambo ya nje wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC ambao kikao chao cha 38 kitafanyika nchini Kazakhstan. Kati ya changamoto muhimu katika kikao hicho ni kutafuta msimamo wa pamoja kuhusu mwamko unaojiri katika nchi kadhaa za OIC.
Mawaziri hao wanatazamiwa pia kuchukua uamuzi kuhusu kikao cha 57 cha viongozi wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu. Mkutano huo uliokuwa umepangwa kufanyika Misri uliakhirishwa kwa sababu ya mwamko wa Kiislamu mwezi Januari nchini humo.
Masuala ya Libya, Pakistan na Somalia yanatazamiwa kutawala ajenda ya OIC na vilevile suala la Afghanistan linatazamiwa kupewa umuhimu. Ajenda nyingine ya kikao hicho ni kubuniwa Tume ya Haki za Binaadamu ya OIC.
Nchi za OIC zinazokumbwa na misukosuko ni pamoja na Yemen, Bahrain, Jordan, Libya na nchini Misri bado hali si shwari.
Kazakhstan ilichukua uenyekiti wa OIC mwaka 2011. Jumuiya ya Nchi za Kiislamu ina wanachama 57.
812523
captcha