IQNA

Rais Ahmadinejad atoa salamu za Ramadhani kwa viongozi wa nchi za Kiislamu

13:03 - August 01, 2011
Habari ID: 2163305
Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametuma salamu za kheri na fanaka kwa viongozi wa nchi za Kiislamu duniani kwa munasaba wa kuanza wezi Mtmukufu wa Ramadhani.
Katika ujumbe wake, Rais Ahmadinejad ameelezea matumaini kuwa katika mwezi huu mtukufu, udugu na umoja utaimarishwa katika umma wa Kiislamu kwa mujibu wa mafundisho ya Qur'ani Tukufu na Suna ya Mtume SAW.
Aidha ameelezea matumaini kuwa mwezi huu mtukufu utakuwa fursa ya kuwatetea waliodhulumiwa ili hatimaye uadilifu na amani ya kudumu ienee duniani.
Rais Ahmadinejad amewatakia afya njema na fanaka viongozi wa nchi za Kiislamu na Waislamu kote duniani.
834933
captcha