IQNA

Sherehe za kuzaliwa Imam Hassan (as) zafanyika kote nchini Pakistan

10:39 - August 19, 2011
Habari ID: 2173065
Sherehe za kuzaliwa Imam Hassan Mujtaba (as) ambaye ni Imam wa pili katika silsila ya Maimamu wa Nyumba ya Mtume (saw) wanaotokana na kizazi cha Mtume Muhammad (saw) zilifanyika Jumanne iliyopita katika pembe zote za Pakistan.
Sherehe hizo zilizotangazwa kuanza rasmi na Hamid Ali Shah Musawi, Kiongozi wa Mashia wa Pakistan, zilifanyika sambamba na kuadhimishwa Siku ya Kimataifa ya Amani katika nchi hiyo.
Mashia wa Pakistan wamemuenzi na kumsifu Imam Hassan Mujtaba (as) katika sherehe hizo zilizofanyika kwa namna mbalimbali kupitia mikutano, seminari, karamu, maonyesho na mikusanyiko. Wasomi, wanafikra na wanazuoni wa Kiislamu walitoa hotuba mbalimbali kusifu na kuzungumzia maisha ya mtukufu huyo wa Nyumba ya Mtume (saw). Hamid Ali Shah Musa alitoa hutuba yake katika mji wa Rawalpindi. 845315
captcha