Taasisi hizo mbili kubwa za Kiislamu nchini Canada zimemtaka Waziri Mkuu wa nchi hiyo kuwaomba radhi Waislamu baada ya kudai kuwa Uislamu ni hatari kwa Canada.
Taarifa la Baraza Kuu la Kiislamu la Canada imekosoa matamshi hayo ya Stephen Harper ikisema kuwa haikubaliki kabisa kwa kiongozi huyo kuufungamanisha Uislamu na makundi yenye misimamo ya kufurutu ada na imemtaka awaombe radhi Waislamu.
Sehemu moja ya taarifa hiyo imesema: "Matamshi ya Waziri Mkuu wa Canada yanawavunjia heshima Waislamu zaidi ya bilioni moja kote duniani."
Kogresi ya Kiislamu ya Canada pia imesema matamshi ya Harper yanawahujumu Waislamu na kwamba alipaswa kutumia maneno yanayofaa kubainisha hatari ya makundi yenye misimamo mikali. 857881