IQNA

Washirika wa Mubarak wazuiwe kushiriki kwenye uchaguzi ujao

15:40 - September 17, 2011
Habari ID: 2188417
Vyama wa siasa nchini Misri vimelitaka baraza la kijeshi linalotawala nchini humo kuwazuia washirika na marafiki wa dikteta wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak kushiriki katika uchaguzi ujao wa bunge.
Muungano wa vyama hivyo ambao unajumuisha vyama 17 vya kisiasa kikiwemo cha Ikhwanul Muslimeen, unataka sheria za uchaguzi zifanyiwe marekebisho na kuwazuia wafuasi wa Mubarak kushiriki kwenye uchaguzi huo.
Umesema unataka kubuniwa kwa sheria ambayo itazuia kikamilifu kurejea madarakani chama cha Mubarak pamoja na wafuasi wake na wakati huohuo kutoa fursa kwa vyama vya kisiasa ambavyo havijahusishwa na uhalifu na jinai dhidi ya taifa la Misri kushiriki kwenye uchaguzi uajo.
Sheria ya sasa ya Misri inatoa fursa kwa wafuasi wa Mubarak kushiriki kwenye uchaguzi kama wagombea huru. 861728
captcha