IQNA

Waziri wa Sheria wa Marekani:

Mafunzo ya kupiga vita Uislamu katika jeshi la Polisi yatakuwa na taathira mbaya

19:15 - November 12, 2011
Habari ID: 2221245
Waziri wa Sheria wa Marekani Eric Holder ameelezea wasiwasi wake mkubwa kutokana na mafundisho ya kupiga vita Uislamu yanayotolewa katika jeshi la polisi la nchi hiyo.
Holder amesema mafundisho yanayotolewa kwa polisi yakieleza kuwa Uislamu ni dini ya kutumia mabavu na ya kikatili si sehemu ya mipango ya masomo ya polisi ya Marekani na kwamba yatakuwa na taathira mbaya na kukwamisha jitihada za kuimarisha maelewano na kuamilia vyema na Waislamu wa nchi hiyo.
Waziri wa Sheria wa Marekani ambaye alikuwa akihutubia Baraza la Seneti la nchi hiyo amesisitiza kuwa, Waislamu wa Marekani ni washirika muhimu katika mapambano dhidi ya ugaidi. Ameongeza kuwa inasikitisha kuona mafundisho kama hayo ya kupiga vita Uislamu yakitolewa katika jeshi la polisi la Marekani.
Septemba mwaka huu gazeti la Wired la Marekani lilifichua kwamba jeshi la polisi la nchi hiyo linapewa mafunzo ya kuupiga vita Uislamu. 896433

captcha