Dakta Ali Larijani ameelezea kusikitishwa kwake na kuaga dunia maafisa kadhaa wa 'Sepah' akiwemo Meja Jenerali Hassan Tehrani Moqaddam, mkuu wa Taasisi ya Jihadi ya Kujitosheleza katika kikosi hicho.
Watu 17 waliepoteza maisha yao kufuatia mlipuko uliotokea jana katika ghala la silaha la Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu magharibi mwa mji mkuu wa Iran, Tehran.
Mkuu wa uhusiano wa umma katika IRGC Luteni Generali Ramezan Sharif amesema watu wengine 16 wamejeruhiwa katika mlipuko huo uliotokea karibu saa saba kamili mchana kwa saa za Tehran. Imearifiwa kuwa mlipuko huo ulitokea wakati silaha zilipokuwa zikibebwa kuelekezwa eneo la oparesheni. Uchunguzi kuhusu chanzo cha mlipuko huo umeanza.
897531