Martin Kobler alizuru Haram ya Imam Ali bin Abi Twalib katika mji mtakatifu wa Najaf jana na kukutana na Ayatullah Ali Sistani.
Mhariri Mkuu wa jarida la Asala Ahmad Abdul Jabbar amesema, baada ya kukutana na Ayatullah Sistan, Martin Kobler alizungumza na waandishi habari na kusema lengo la safari yake mjini Najaf lilikuwa kuzuru Haram ya Imam Ali bin Abi Twalib na kuadhimisha mji huo mtakatifu na nafasi yake ya kimaanawi.
Katika mazungumzo yake na waandishi habari mjumbe huyo wa Umoja wa Mataifa alichunguza matatizo ya kisiasa, kijamii na masuala ya ustawi ya Iraq na vilevile hali ya baada ya kuondoka askari vamizi wa Marekani nchini humo. 903262