IQNA

Kongamano la ‘Utandawazi na Dini’ nchini Algeria

16:41 - November 23, 2011
Habari ID: 2227218
Kongamano la Kimataifa kuhusu ‘Dini na Utandawazi’ limefanyika kati ya Novemba 22-23 nchini Algeria mjini Algiers.
Ammar Mosa’edi Mkuu wa Kitivo cha Sayansi za Kiislamu katika Chuo Kikuu cha Algeria amemwambia mwandishi wa IQNA kuwa kongamano hilo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya vyuo vikuu vya Tehran na Algeria.
Kongamano hilo limehutubiwa na wasomi sita kutoka Algeria pamoja na wanazuoni wa Kishia na Kisuni kutoka Iran, Tunisia, Syria, Misri, Sudan, Qatar na Amerika.
Kongamano hilo limejadili masiala kama vile, ‘dini na zama za utandawazi’, ‘nafasi ya fiqhi ya Kiislamu katika utandawazi’, na ‘familia na mwanamke katika utandawazi’.
902209
captcha