IQNA

Gabon, mwenyeji wa mkutano wa 9 wa Mawaziri wa Habari wa nchi za Kiislamu

19:30 - December 14, 2011
Habari ID: 2238942
Mkutano wa 9 wa Mawaziri wa Habari wa nchi wanachama wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) umepangwa kufanyika Libreville, mji mkuu wa Gabon.
Katibu Mkuu wa OIC Ekmeleddin Ihsanoglu ameuambia ujumbe wa Gabon kwamba hii itakuwa mara ya kwanza kwa mkutano huo wa Mawaziri wa Habari wa nchi za Kiislamu kufanyika nchini humo.
Ujumbe huo wa Gabon umeeleza mipango na maandalizi yaliyofanyika hadi sasa kwa ajili ya mkutano huo.
Ujumbe huo pia umejadiliana na kubadilishana mawazo na maafisa wa ngazi za juu wa OIC kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu mkutano huo.
Mkutano huo utaanza tarehe 18 hadi 21 Aprili mwakani. 915504


captcha