IQNA

Wapinzani wa Aal Saud kufanya zilzala Ijumaa ijayo

20:10 - January 04, 2012
Habari ID: 2251498
Muungano wa "Watu Huru wa Qatif" umetoa taarifa ukiitangaza Ijuma ijayo kuwa ni "Siku ya Zilzala ya Watu Huru" na umetoa wito wa kufanyika maandamano makubwa dhidi ya hukumu ya kutiwa nguvuni Waislamu 23 wa madhehebu ya Shia nchini humo.
Kanali ya televisheni ya al Alam imeripoti kuwa, wananchi wa Saudi Arabia wana misimamo tofauti kuhusu hukumu iliyotolewa na vyombo vya serikali ya kutiwa nguvuni Mashia 23 kwa sababu ya kushiriki kwenye maandamano dhidi ya serikali katika eneo la Alsharqiyya.
Muungano huo umesema: Mashia hao 23 ambao wametambuliwa na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Saudia kuwa ni wahalifu na imetoa hukumu ya kutiwa kwao nguvuni, ni sehemu ya jamii ya Mashia wa Saudi Arabia ambao wanataka kurejeshewa haki zao zilizoghusubiwa.
Muungano wa Watu Huru umesema, tuhuma zilizotolewa na utawala wa Aal Saud dhidi ya raia hao ni za bandia na za kidhalimu.
Muungano huo umewataka wakazi wa Qatif kushiriki kwa wingi katika maandamano ya Siku ya Zilzala ya Watu Huru yatakayofanyika Ijumaa ijayo kwa ajili ya kuonyesha malalamiko yao dhidi ya hatua hiyo ya serikali ya Saudi Arabia. 928852


captcha