Kundi la Waislamu kwa Ajili ya Amani limetangaza katika maandamano hayo kwamba kitendo hicho cha kuzuiwa vazi la hijabu kinaakisi chuki na uhasama dhidi ya Uislamu.
Kitendo hicho pia kinapingana na sheria za Wizara ya Elimu ya Thailand inayowapa Waislamu wa kike haki ya kuvaa hijabu mashuleni.
Taarifa ya kundi hjilo imesema baadhi ya walimu wa shule hiyo wamekuwa wakijizuia kumfunza binti huyo anayevaa hijabu wa Kiislamu.
Waislamu hao wa Thailand wamemtaka Waziri Mkuu wa nchi hiyo kuingilia kati na kutatua kadhia hiyo. 933058