IQNA

Mufti wa Quds aonya kuhusu njama dhidi ya Msikiti Mtakatifu wa al-Aqsa

9:52 - March 11, 2012
Habari ID: 2289168
Mufti wa Quds na ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina amesisitiza juu ya udharura wa kuungwa mkono msikiti wa al-Aqsa mkabala na njama hatari za utawala wa Kizayuni wa Israel. Amesema njama hizo ni pamoja na kuibua mtetemeko bandia wa ardhi kwa lengo la kuuharibu Msikiti wa Al Aqsa.
Sheikh Muhammad Hussein, Khatibu wa Masjidul Aqsa amesema kuwa, amewataka Waislamu kote ulimwenguni kuuhami msikiti huo mtakatifu na kibla cha kwanza cha Waislamu unaoandamwa na njama za maadui Wazayuni.
Aidha amewataka Waislamu kwenda kufanya ibada zao katika msikiti huo na amepinga vikali fatuwa zinazowazuia wasiokuwa Wapalestina kutembelea Quds.
Sheikh Muhammad Hussein ameashiria nafasi ya Misri katika kuihami Quds na Msikiti wa al-Aqswa na kusisitiza kwamba, hatua zozote zile dhidi ya msikiti huo mtakatifu zitahatarisha usalama wa taifa wa Misri.
Wakati huo huo, Mufti wa Quds na ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina amezitaka Hamas na Fat'h kuhitimisha hitilafu zao za ndani na badala yake kudumisha umoja na mshikamano.
969063
captcha