Akizungumza hapo jana Jumatatu, Miqaati alisema kuwa kuna baadhi ya mirengo nchini Lebanon ambayo ina wasiwasi kuhusiana na silaha za Hizbullah lakini ameitaka kuwa na utulivu kwa kuiambia kwamba silaha hizo kamwe hazitatumika dhidi yao.
Waziri Mkuu wa Lebanon amekaribisha wito uliotolewa hivi karibuni na Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah wa kuitaka mirengo na makundi yote ya kisiasa ya Lebanon yakutane na kufanya mazungumzo ya kuimarisha umoja na mshikamano nchini.
Akiashiria ghasia za hivi karibuni nchini humo Miqaati amesema kuwa, kuna mikono ya kigeni inayojaribu kuzusha fitina na vurugu nchini humo lakini akaongeza kuwa moto wa fitina hiyo umezimwa kutokana na hatua za kimantiki zilizochukuliwa na serikali pamoja na taifa la Lebanon. 1028145