IQNA

Waenezaji wa hofu dhidi ya Uislamu wana lengo moja na wanoupiga vita Uyahudi

19:52 - June 13, 2012
Habari ID: 2346232
Utafiti uliofanywa hivi karibuni na Chuo Kikuu cha California nchini Marekani umebaini kwamba wanaoeneza woga na hofu dhidi ya Uislamu wana malengo mamoja na wanaopiga vita Uyahudi katika nchi za Magharibi.
Kwa mujibu wa tovuti ya trouvetamosquee, utafiti na uchunguzi huo unaonesha kwamba watu wanaojiarifisha katika nchi hizo kuwa wapinzani wa Uyahudi ndio walewale wanauopiga vita Uislamu.
Ripoti ya utafiti huo inaoonyesha kwamba Waislamu na Mayahudi wanaopigwa vita na kubaguliwa katika nchi za Magharibi wana hisia inayofanana kuhusiana na suala hilo, jambo ambalo taratibu linaimarisha umoja na mshikamano kati yao.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo Waislamu na Mayahudi wamekuwa wakiandaa makongamano na mijumuiko ya pamoja kwa lengo la kupanga mikakati ya pamoja ya kukabiliana na chuki na ubaguzi dhidi yao. 1029006
captcha