Majlisi hiyo imemwandikia barua Waziri Mkuu na Waziri wa Habari wa India ikiwataka waingilie kati na kusimamisha mara moja utengenezaji wa filamu hiyo kwa sababu inadhuru hisia za Waislamu. Akitoa taarifa kuhusiana na suala hilo, Maulana Reza Muhammad At'har mkuu wa majlisi hiyo amesema kutokana na kuwa sifa za Imam Hussein (as) ambaye anaenziwa na kutukuzwa na mamilioni ya Waislamu duniani zitazungumziwa katika filamu hiyo na kupelekea kudhuriwa hisia zao, majlisi hiyo inaitaka serikali iingilie kati mara moja na kusimamisha utengenezaji wake. Amesema kwa mtazamo wa sheria za Kiislamu, utengenezaji wa filamu kama hiyo inayowahusu watu mashuhuri na watukufu wa kidini ni jambo lisiloruhusiwa. 1056878