IQNA

Ofisi ya Allama Fadhlullah yatangaza Jumapili kuwa siku ya Idul Fitr

13:30 - August 14, 2012
Habari ID: 2392782
Ofisi ya marehemu Allama Muhammad Hussein Fadhlullah wa Lebanon imetangaza kuwa siku ya Jumapili tarehe 19 Agosti itakuwa siku ya kwanza ya mwezi wa Shawal na hivyo kuwa siku ya sikuu ya Idul Fitr.
Kwa mujibu wa tovuti ya lorientlejour, Kamati ya Masuala ya Kisheria ya Taasisi ya Allama Muhammad Hussein Fadhlullah jana ilitoa taarifa ikisema kuwa kwa kuzingatia kuwa siku ya Jumapili itakuwa siku ya Idi, siku ya mwisho ya Mashia kufunga itakuwa siku ya Jumamosi tarehe 18 Agosti.
Kwa upande wa pili, Darul Fatawa ya Lebanon ambayo ndiyo taasisi kuu inayoshughulika masuala ya sheria za Kiislamu nchini humo kwa Masuni, hadi sasa haijatangaza siku rasmi ya kusherehekewa Idul Fitr na kwa hivyo wafuasi wa madhehebu hiyo wangali wanasubiri kutangazwa kwa siku hiyo. 1078305
captcha