IQNA

Nakala za Qur’ani za hati za braille zasambazwa katika nchi za Kiislamu

21:37 - September 03, 2012
Habari ID: 2404343
Nakala za Qurani zenye hati za braille (hati zinazotumiwa na walemavu wa macho au vipofu) zimesambazwa bure nchini Saudi Arabia na katika nchi nyingine za Kiislamu kwa juhudi za Jumuiya ya Masuala ya Kheri na Huduma za Walemavu wa Macho.
Gazeti la al Riyadh linalochapishwa nchini Saudi Arabia limemnukuu Mwenyekiti wa Baraza la Idara la Jumuiya hiyo Bwana Ahmad Muhammad Ali akisema kuwa mpango wa kusambaza nakala za Qur’ani zenye hati za braille unatekelezwa kwa ushirikiano wa taasisi na vituo kadhaa vinavyotoa huduma kwa walemavu wa macho.
Ahmad Muhammad Ali ameongeza kwamba lengo la kutekeleza mpango huo ni kuwawezeshawalemavu wa macho kusoma Qur’ani kwa hati za braille.
Ameongeza kuwa imepangwa kuwa vituo vya Qur’ani vya ulimwengu wa Kiislamu vitashirikiana kuchapicha vitabu vya tafsiri ya Qur’ani na vya sira ya Mtume Muhammad (saw) kwa hati za braille katika kiwanda cha kuchapisha Qur’ani cha Mfalme Fahad nchini Saudi Arabia. 1090377
captcha