Mashindano hayo ambayo mwaka huu yatahusu hifdhi ta Qur'ani yatasimamiwa na Rais wa Baraza la Mamufti la Russia Ravi Ainuddin kwa msaada wa Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo.
Mashindano hayo yatafanyika katika awamu mbili na mahafidhi bora watakaofaulu vizuri katika awamu ya awali watachuana katika awamu ya pili na ya mwisho.
Mahafidhi 30 kutoka nchi mbalimbali ikiwemo Uturuki, Ufaransa, Qazakhstan, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Saudi Arabia, Marekani, Indonesia, Tunisia, Afrika Kusini, China na Morocco watashiriki katika mashindano hayo.
Watayarishaji wa mashindano ya 13 ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu nchini Russia wametayarisha ratiba mbalimbali zitakazofanyika katika mashindano hayo. 1093478