Maandamano hayo yamefanyika kuonyesha mshikamano na umoja wa Waislamu hao na ndugu zao wa madhehebu ya Shia.
Katika maandamano hayo ya Waislamu wa madhehebu ya Suni maulamaa wa dini wa Pakistan wamewataka maafisa wa serikali kuhakikisha uadilifu unatendeka na kusema Waislamu wa Shia na Suni wa Pakistan wanaungana katika kulinda nchi yao na wanaelewa vyema njama zinazofanywa na maadui.
Wamesisitiza kuwa njama hizo zinazopangwa na mabeberu na nchi zinazopinga Uislamu dhidi ya wafuasi wa dini hiyo hazitafaulu. 1093464