Maandamano hayo yameitishwa na Kituo cha Kiislamu cha Marekani kwa lengo la kukabiliana na chuki na kueneza amani, nia njema na urafiki.
Maafisa wa Kituo cha Kiislamu cha Marekani wametangaza kuwa malengo mengine ya maandamano hayo ni kutoa mafunzo kuhusu Uislamu na utamaduni wa nchi za Waislamu.
Alkhamisi iliyopita pia viongozi wa dini mbalimbali na viongozi wa serikali wa eneo hilo walifanya maandamano mbele ya ofisi za Kituo cha Kiislamu wakipinga vitendo vya kumvunjia heshima Mtume wa Mwenyezi Mungu.
Waandamanaji hao walishikana mikono kama ishara ya umoja na mshikamano na kutangaza upinzani wao dhidi ya juhudi zinazofanywa kwa ajili ya kueneza chuki na uhasama wa kidini. 1104207