IQNA

Dola laki moja zatengwa kwa atakayemuua mtayarishaji wa filamu chafu ya Kimarekani

15:19 - September 23, 2012
Habari ID: 2417908
Waziri wa Reli wa Pakistan ametenga zawadi ya dola laki moja kwa mtu yeyote atakayemuua mtayarishaji wa filamu inayomdhalilisha Mtume Muhammad (saw).
Waziri wa Reli wa Pakistan Ghulam Ahmad Bilor amewaambia waandishi habari kwamba atampa zawadi ya dola laki moja mtu yeyote atakayemuua mtayarishaji wa filamu ya Innocence of Muslims.
Amesema: Nikimpata mtu huyo aliyetengeneza filamu inayomdhalilisha Mtume (saw) nitamuua mimi mwenyewe na baadaye nitakuwa tayari kunyongwa.
Maandamano ya kupinga filamu inayomvunjia heshima Mtume Muhammad (saw) yanaendelea kufanyika katika nchi mbalimbali duniani. 1104628
captcha