Katibu Mkuu wa OIC Ekmeleddin Ihsanoglu ameashiria maazimio hayo ya Umoja wa Mataifa na kusema kuwa sheria hizo zinapaswa kutekelezwa.
Amesema kuwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa na Baraza la Haki za Binadamu yalipasisha sheria zinazopiga marufuku kuvunjiwa heshima matukufu ya kidini.
Ihsanoglu amesema hayo siku kadhaa baada ya mawaziri wa mambo ya nje wa nchi za Kiislamu kutoa taarifa wakilaani filamu ya Kimarekani inayomvunjia heshima Mtume Muhammad (saw).
Taarifa hiyo ilisema kuwa filamu hiyo inachochea uhasama, ubaguzi na uadui dhidi ya Waislamu, dini ya amani ya Uislamu na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). 1111314