IQNA

Mkristo ashika nafasi ya pili mashindano ya Qur'ani Misri

16:43 - October 02, 2012
Habari ID: 2424665
Mkristo wa Misri Majdi al Gheiti mwenye umri wa miaka 38 ameshika nafasi ya pili katika mashindano ya Qur'ani Tukufu yaliyosimamiwa na Maktaba Kuu ya eneo la al Muusara nchini humo.
Hazeti la al Masri al Youm limeripoti kuwa, Majdi al Gheiti ambaye alikuwa mshindani Mskristo katika mashindano hayo amefanikiwa kushika nafasi ya pili. Mkristo huyo amechuana na washiriki wengine 19 ambao wote walikuwa Waislamu.
Al Gheiti amesema kuwa katika mashindano hayo ya maandishi ametumia masaa manne kujibu maswali 20 yanayohusiana na Qur'ani na kushika nafasi ya pili.
Majdi al Gheiti amesema kuwa lengo la kushiriki katika mashindano hayo ya Qur'ani ni kuonesha udugu na umoja kati ya Waislamu na Wakristo nchini Misri na kulidhihirisha eneo la al Muusara kuwa nembo na kigezo bora cha kuisha kwa amani kati ya raia Wakristo na wenzao Waislamu. 1111681

captcha