IQNA

Duru ya 14 ya mashindano ya kitaifa ya Qur'ani Tukufu yafanyika Yemen

16:06 - October 03, 2012
Habari ID: 2425339
Duru ya 14 ya mashindano ya kitaifa ya Qur'ani Tukufu kwa ajili ya vijana ilianza jana Jumanne huko Sanaa mji mkuu wa Yemen.
Sheikh Yahya al-Halili, MuhamMad Jam'an na Swadiq Abdallah wamesimamia visomo vya makarii 33 wa kitaifa ambao walisoma Qur'an kwa visomo tofauti.
Fuad ar-Ruhani, mmoja wa wasimamizi wa mashindano hayo amesema kuwa makarii 50 wa Yemen wameshiriki katika mashindano hayo ambayo yamepangwa kumalizika leo Jumatano.
Washindi wa mashindano hayo pamoja na wengine walioshiriki katika mashindano ya miaka ya 2010 na 2011 wanatazamiwa kupewa zawadi zao katika sherehe maalumu ambayo imepangwa kufanyika mwishoni mwa mwaka huu. 1112621
captcha