Waziri wa Afya wa Mauritius alianza kushughulikia suala hilo baada ya wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Hospitali ya Victoria katika mji wa Port Louis kuwasilisha mashtaka dhidi ya wasimamizi wa chuo hicho kwa sababu ya kuzuia vazi la hijabu.
Waziri wa Afya wa Mauritius amesema kuwa tatizo la wanafunzi wa chuo cha wauguzi limetatuliwa na tangu sasa wanaweza kwenda kazini wakiwa na vazi la hijabu.
Ameongeza kuwa hakuna sheria yoyote inayopiga marufuku vazi la hijabu katika maeneo ya kazi.
Waziri wa Kazi wa Mauritius pia amekosoa hatua za kuzuia vazi la hijabu mahospitalini na katika vituo vya umma na ametaka sheria zote kuhusu suala hilo zitazamwe upya. 1121617