IQNA

Mashindano ya kimataifa ya Qur'ani kuanza leo Saudia

8:49 - December 02, 2012
Habari ID: 2456759
Mashindano ya 34 kimataifa ya hifdhi, tajwidi na tafsiri ya Qur'ani yanaanza leo nchini Saudi Arabia yakiwashirikisha makarii kutoka nchi 53 katika Masjidul Haram mjini Makka.
Mashindano hayo ambayo yamepewa jina la Mashindano ya Mfalme Abdul Aziz yanasimamiwa na Wizara ya Wakfu ya Saudia yakiwashirikisha makarii 164 kutoka nchi 53.
Viongozi wa Saudi Arabia hawakuwaalika makarii wa Qur'ani kutoka Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa mwaka wa pili mfululizo.
Viongozi wa Jumuiya ya Wakfu ya Iran wanasema kutoalikwa wasomaji Qur'ani wa Iran kunatokana na ama masuala ya kisiasa au uwezo mkubwa wa makarii wa Jamhuri ya Kiislamu, kwani maafisa wa Saudia hawataki kuona Wairani wakishinda mashindano hayo. 1146279



captcha