Sheikh wa al Azhar amesema Uislamu umekataza kuua nafsi isiyo na hatia na imeharamisha kuchoma moto nafsi katika hadhara au kwa njia yoyote ya kidhalimu hata katika vita na adui mvamizi. Amesema kitendo cha kundi la Daesh ni uovu unaopigwa vita na dini zote
Tarifa ya Sheikh Mkuu wa al Azhar imesema wanachama wa Daesh ni mafisadi na waharibifu katika ardhi ambao wanapigana vita dhidi ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kwa msingi huo wanapaswa kuadhibiwa. Sheikh al Tayyib ameitaka jamii ya kimataifa kukabiliana vilivyo na kundi hilo la kigaidi lililofanya jinai za kutisha. AIR 2808398