IQNA

Shirika la Bin Ladin lalaumiwa kufuatia kuanguka kreni Makka

15:42 - September 16, 2015
Habari ID: 3363334
Idara ya Mfalme wa Saudi Arabia, Salman bin Abdul Aziz imelizuia shirika la ujenzi la Bin Ladin kuendelea na shughuli zake za ujenzi nchini humo baada ya kutokea ajali ya kreni auwinchi iliyopelekea zaidi ya mahujaji 107 kufariki dunia mjini Makka.

Salman amelizuia shirika hili kuchukua kandarasi yoyote ya ujenzi na kumwamuru waziri wa fedha wa Saudia kuangalia upya kandarasi lilizo nazo hivi sasa shirika hilo la Binladin.
Kwa mujibu wa amri hiyo, maafisa wote waandamizi wa shirika hilo pamoja na wajumbe wa bodi ya Bin Ladin Group wamepigwa marufuku kusafiri nje ya Saudia mpaka uchunguzi kuhusu ajali hiyo utakapokamilika.
Kamati ya kuchunguza ajali hiyo imetoa ripoti na kusema katika sehemu moja ya ripoti yake kuwa, shirika la Bin Ladin Group linapaswa kulaumiwa kwa namna fulani, kutokana na ajali hiyo ya kutisha.
Mfalme wa Saudia pia ametoa amri ya kulipwa dola 267,000 kwa kila familia ya wahanga wa ajali hiyo na karibu ya nusu ya fedha kama hizo watalipwa mahujaji waliojeruhiwa.

3363017

Kishikizo: kreni makka binladin ajali
captcha