Taarifa kuhusu mashindano hayo imetolewa na Kituo cha Masomo ya Kiislamu katika Chuo Kikuu cha Usmanu Danfodiyo jimboni Sokoto.
Akizungumza na waandishi habari, Dkt. Sani Yusuf Birin Tudu mratibu wa kitaifa wa mashindano hayo amesema awali ilikuwa imepangwa yaanzi Januari 8 lakini yakasongezwa mbele zaidi.
Waandalizi wa mashindano hayo wamebainisha masikitiko yao kufuatia kuahirishwa na kusema ilitokana na sababu ambazo hazingeweza kuepukika.