
Mzayuni huyo aliyekuwa na misimamo ya kufurutu ada aliwashambulia na
kuwamiminia risasi Waislamu waliokuwa wakitekeleza ibada ya Swala katika
Msikiti wa Haram ya Nabii Ibrahim mjini al Khalil, Palestina inayokaliwa kwa
mabavu na kuua shahidi 29 miongoni mwao. Mauaji hayo yalitokea wakati Waislamu
hao walipokuwa katika ibada ya funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhani. Waislamu
wengine wengi walijeruhiwa katika shambulizi hilo la kikatili.
Mauaji hayo ambayo yalidhihirisha tena uhasama na chuki za Wazayuni wa Israel
dhidi ya Waislamu, yalilaaniwa na Waislamu kote duniani. Ukatili huo ulizusha
wimbi kubwa la machafuko katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina
ambapo wananchi walizidisha mapambano dhidi ya maghasibu wa Tel Aviv. Israel
ilimshika kwa muda na kumuachia huru mhalifu huyo katili kwa kisingizio kwamba
alikuwa punguani!
3478239