Katika sehemu nyengine ya hotuba yake, Ayatullah Muhammad Ali Movahedi-Kermani amesema kuna ulazima wa vikosi vya ulinzi kujizatiti kwa silaha za kisasa kwa ajili ya kukabiliana na vitisho vya maadui.
Aidha ameashiria vitisho vya maadui dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kueleza kwamba katika mazingira kama hayo ni jambo la lazima kwa vikosi vya ulinzi kujizatiti kwa silaha; na suala hilo halina uhusiano na nchi yoyote.
Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya Tehran amegusia ubabe na utumiaji mabavu unaofanywa na Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati na kusisitiza kuwa Marekani haiwezi kuizuia Iran isijizatiti kwa silaha za kisasa.
Aidha amelaani jinai zinazofanywa na utawala wa Aal Saud na utawala wa Kizayuni katika eneo hili na kuongeza kuwa Marekani inazipatia tawala hizo silaha zake angamizi ili zizitumie kwa ajili ya kuwaulia Waislamu.
Ayatullah Movahedi-Kermani amesema misimamo potofu ya Marekani katika Mashariki ya Kati ndio sababu ya machafuko na ukosefu wa amani unaoshuhudiwa katika eneo na akongezea kwa kusema, misimamo hiyo inasababisha madhara kwa nchi za eneo hili.