TEHRAN (IQNA) - Siku kama ya leo miaka 26 iliyopita, February 25, 1994, Mzayuni mmoja aliyekuwa na misimamo ya kufurutu ada aliwashambulia na kuwamiminia risasi Waislamu waliokuwa wakitekeleza ibada ya Swala katika Msikiti wa Haram ya Nabii Ibrahim mjini al Khalil (Hebron), Palestina inayokaliwa kwa mabavu na kuua shahidi 29 miongoni mwao.

Mauaji hayo, yaliyotekelezwa na malowezi wa Kizayuni Baruch Goldstein aliyekuwa daktari katika jeshi la Israel, yalitokea wakati Waislamu hao walipokuwa katika ibada ya funga ya mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Waislamu wengine wengi walijeruhiwa katika shambulizi hilo la kikatili.Mauaji hayo ambayo yalidhihirisha tena uhasama na chuki za Wazayuni wa Israel dhidi ya Waislamu, yalilaaniwa na Waislamu kote duniani.
Ukatili huo ulizusha wimbi kubwa la machafuko katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina ambapo wananchi walizidisha mapambano dhidi ya maghasibu wa Tel Aviv. Israel ilimshika kwa muda na kumuachia huru mhalifu huyo katili kwa kisingizio kwamba alikuwa punguani!