israel

IQNA

IQNA – Umoja wa Kimataifa wa Wanazuoni wa Kiislamu (International Union of Muslim Scholars – IUMS) umetoa fatwa (hukumu ya kidini) ikitangaza kwamba kuwa na mahusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel ni haramu kisheria kwa mujibu wa Uislamu.
Habari ID: 3481830    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/21

IQNA – Katibu Mkuu wa Jukwaa la Kimataifa la Umoja na Kukurubisha Madhehebu ya Kiislamu (WFPIST) amesisitiza haja ya kuimarisha umoja na kudumisha umakini wa ulimwengu wa Kiislamu kuhusu suala la Palestina.
Habari ID: 3481825    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/20

IQNA-Ripoti ya pamoja ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu ya Palestina imeripoti kuwa, kuanzia Oktoba 2023 hadi Oktoba 2025, walimu wasipungua 1,377 na wafanyakazi wa elimu waliuawa shahidi na 4,757 wamejeruhiwa katika mauaji ya kimbari yanayotekelezwa na utawala dhalimu wa Israel huko Gaza.
Habari ID: 3481824    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/20

IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, kuhusika moja kwa moja Marekani, utawala wa Kizayuni na baadhi ya nchi za Ulaya katika matukio ya hivi karibuni ya Iran hakukanushiki.
Habari ID: 3481809    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/17

IQNA – Utawala ghasibu wa Israel umetangaza mipango ya kuweka vizuizi kwa waumini Waislamu wanaotaka kufika Msikiti wa Al-Aqsa katika mji mtakatifu wa al-Quds (Jerusalem0, wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3481807    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/15

IQNA-Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) amezionya Marekani, Israel na mamluki wao wenye mienendo ya kigaidi kama ile ya Daesh kwamba kosa lolote la kimahesabu litakabiliwa na majibu makali na ya kuangamiza.
Habari ID: 3481805    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/15

IQNA – Akizungumzia machafuko yanayodaiwa kuungwa mkono na Israel katika miji ya Iran, Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki alisema kuwa malengo ya utawala wa Israel ndani ya Iran hayatoweza kutimia. Hakan Fidan amesisitiza kuwa utawala wa Tel Aviv hautafanikiwa katika njama zake dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
Habari ID: 3481794    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/12

IQNA- Kikao cha Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) kilichojadili suala la Somalia na hatua ya utawala wa Kizayuni ya kulitambua eneo la nchi hiyo la Somaliland, kama nchi huru kimefanyika katika makao makuu ya jumuiya hiyo mjini Jeddah, Saudi Arabia.
Habari ID: 3481790    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/11

IQNA – Maelfu ya waandamanaji walijitokeza Ijumaa katika mji mkuu wa Morocco kupinga hatua ya nchi hiyo ya kuendeleza uhusiano wa kawaida na utawala wa Kizayuni wa Israel.
Habari ID: 3481788    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/11

IQNA-Rais Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia amezinukuu ripoti za kiitelijinsia na kusema kuwa eneo lililojitenga la na nchi hiyo la Somaliland limekubali kuwapokea Wapalestina na kuanzishwa kambi ya kijeshi ya Israel katika eneo hilo mkabala wa kutambuliwa rasmi na Israel.
Habari ID: 3481750    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/01

IQNA-Hatua ya kichokozi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kutambua eneo la Somalia la 'Somaliland' kama nchi huuru kunahusishwa na mradi mpana zaidi wa kuchora upya ramani ya ushawishi katika Pembe ya Afrika na Bahari Nyekundu, mradi unaoendeshwa kwa misukumo ya kiusalama kwa ushirikiano wa utawala wa Israel na pia Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE).
Habari ID: 3481748    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/01

IQNA-Wakipita njia zilizozungukwa na majengo yaliyoharibiwa na vifusi, wanafunzi Wapalestina wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Gaza wiki hii wamerudi darasani kwa mara ya kwanza baada ya miaka miwili.
Habari ID: 3481692    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/21

IQNA – Mkuu wa Shirika la Utangazaji la Umma nchini Uhispania (RTVE), José Pablo López, amemkemea Mkurugenzi wa Mashindano ya Muziki ya Eurovision kwa barua yake ya wazi kwa mashabiki ambayo haikutaja Gaza wala utawala wa Israel, akisema hatua hiyo ni “kushindwa” wakati mashindano hayo yanapitia mgogoro mkubwa wa kiheshima.
Habari ID: 3481653    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/13

IQNA-Kiongozi wa Harakati ya Ansarullah nchini Yemen, Abdul‑Malik al‑Houthi, amelaani vikali ukatili unaofanywa na utawala wa Kizayuni dhidi ya wanawake wa Palestina, akisema maelfu ya wanawake—akiwemo wajawazito, wasichana wadogo na wazee—wameuawa katika maeneo yote yanayokaliwa kwa mabavu.
Habari ID: 3481649    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/12

IQNA – Harakati ya mapambano ya Hizbullah nchini Lebanon imemtaka Kiongozi wa Kanisa Katoliki kulaani ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha vita na mashambulizi ya Israel dhidi ya taifa hilo la Kiarabu.
Habari ID: 3481592    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/30

IQNA – Makamu wa Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Hussein al-Sheikh, amesifu tamko la pamoja la Ufaransa, Ujerumani, Italia na Uingereza lililolaani kuongezeka kwa mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi.
Habari ID: 3481581    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/28

Maoni
IQNA-Afisa wa zamani wa utawala wa Kizayuni wa Israel amefichua kuwa taarifa za kijasusi za Israel zilichochea mapigano ya Darfur, Sudan ili kuisukuma hali kuelekea kwenye mgogoro na mgawanyiko zaidi, na kwamba mapigano ya sasa nchini humo hatimaye yataishia kwa kugawanywa katika maeneo kadhaa.
Habari ID: 3481576    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/27

IQNA – Mufti Mkuu wa Oman ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa na nchi za Kiislamu kuushinikiza utawala wa Kizayuni kusitisha ukiukaji wa makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
Habari ID: 3481527    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/17

IQNA – Katika kura ya maamuzi yenye uzito, Shirikisho la Soka la Ireland (FAI) limeunga mkono azimio linaloitaka UEFA kuifukuza Israel kutoka kwenye mashindano ya kimataifa na ya vilabu barani Ulaya.
Habari ID: 3481491    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/11/09

IQNA – Mfungwa wa Kipalestina aliyeachiliwa kutoka gereza la utawala wa Kizayuni ameeleza mateso makali na hali isiyo ya kibinadamu inayowakumba wafungwa wa Kiislamu, ikiwemo udhalilishaji wa Qur'an Tukufu na kuzuia adhana na sala za jamaa.
Habari ID: 3481418    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/10/26