IQNA

Qiraa ya Qur’ani Tukufu ya mwanae Ustadh Abdul Basit kuhusu Ramadhani

16:06 - May 06, 2020
Habari ID: 3472739
TEHRAN (IQNA) – Sheikh Tariq Abdul Basit Abdul Samad, mwanae qarii mashuhuri wa Qur’ani Tukufu nchini Misri marhum Sheikh Abdul Basit Abdul Samad, hivi karibuni amesoma aya za Qur’ani Tukufu kuhusu Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.

Katika video hii, Sheikh Tariq anasoma aya ya 185 ya Surah al-Baqara ya Qur’ani Tukufu isemayo: “ Mwezi wa Ramadhani ambao imeteremshwa humo Qur'ani kuwa ni uwongofu kwa watu, na hoja zilizo wazi za uwongofu na upambanuzi. Basi ataye kuwa mjini katika mwezi huu naafunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi atimize hisabu katika siku nyengine. Mwenyezi Mungu anakutakieni yaliyo mepesi wala hakutakieni yaliyo mazito, na mtimize hiyo hisabu, na mumtukuze Mwenyezi Mungu kwa kuwa amekuongoeni ili mpate kushukuru.”

Taqriq ni kati ya watoto 10 wa marhum Sheikh Abdu Basit. Katika mahojiano aliyowahi kufanya huko nyuma alisema baba yake alisisitiza kuwa yeye na ndugu zake wote wahifadhi Qur’ani Tukufu. Tariq alihifadhi  Qur’ani kikamilifu akiwa na umri wa miaka 15 na baada ya hapo akawa qarii mashuhuri kama alivyokuwa baba yake.

3896497

captcha