IQNA

Mfawidi wa Haram takatifu ya Hazrat Abbas (AS) kuandaa ibada za maombolezo ya Muharram barani Afrika

18:20 - July 15, 2024
Habari ID: 3479125
IQNA - Idara ya Mfawidhi wa Kaburi (Haram) takatifu ya Hazrat Abbas (AS) nchini Iraq imeandaa maombolezo katika nchi za Kiafrika wakati wa mwezi wa Hijri wa Muharram.

Idara ya Masuala ya Kiakili na Utamaduni ya Mfawidhi wa  Kaburi (Haram) takatifu ya Hazrat Abbas (AS) nchini Iraq imeandaa mipango hiyo kila mwaka, kulingana na tovuti ya Al-Kafeel. 

Sayyed Muhsin al-Jbiri, afisa wa idara hiyo, alisema programu hizo zinalenga kukuza utamaduni wa Imamu Husseini (AS) na kuongeza ufahamu kuhusu harakati ya Imam Hussein (AS).

Zinafanyika katika nchi kama Nigeria, Tanzania, Mauritania, Senegal, Ghana, Madagascar, Kenya, Rwanda, Niger, Benin, Cameroon, na Sierra Leone, alibainisha.

Moja ya maombolezo hayo katika mji wa Kaduna, Nigeria, zilihudhuriwa na idadi kubwa ya wafuasi wa Ahl-ul-Bayt (AS) wiki hii.

Akitoa hotuba katika hafla hiyo, Sheikh Ibrahim Yusuf Musa alibainisha fadhila za kulilia matukio ya kusikitisha aliyopitia Imam Hussein (AS).

3489123

captcha