IQNA

Dunia yapongeza makubaliano ya nyuklia ya Iran

11:26 - November 26, 2013
Habari ID: 1323865
Nchi tofauti mbalimbali zimepongeza makubaliano yaliyofikiwa hivi karibuni kati ya Iran na madola 6 yenye nguvu duniani kuhusiana na shughuli zake za nishati ya nyuklia. Pakistan imekaribisha makubaliano hayo ambapo Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi hiyo imesema, Pakistan ikiwa nchi ndugu na jirani na Iran siku zote imekuwa ikisisitiza umuhimu wa kadhia hiyo kutafutiwa suluhusho la amani. Uturuki pia imekaribisha makubaliano hayo ya nyuklia kati ya Iran na kundi la 5+1 na Rais Abdallah Gul wa nchi

Naye Omran al Zoubi Waziri wa Habari wa Syria amesema makubaliano hayo ya kihistoria ni ushindi wa kutumiwa mantiki ya mazungumzo na njia za kisiasa dhidi ya vitisho, changamoto na vita. Kuwaiti pia imekaribisha makubaliano hayo yaliyofikiwa kati ya Iran na nchi 5 wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pamoja na Ujerumani. Iraq, Uturuki, Bahrain, Umoja wa Falme za Kiarabu  na Jordan pia zimetangaza kuunga mkono makubaliano ya nyuklia ya Iran.

Wakati huo huo Ufaransa imesema kuwa, kuna uwezekano mwezi Disemba Umoja wa Ulaya ukaiondolea Iran baadhi ya vikwazo kufuatia makubaliano yaliyofikiwa kati ya Tehran na nchi za Magharibi. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban ki-Moon pia ametoa tamko na kupongeza makubaliano ya nyuklia kati ya Iran na madola matano yenye nguvu duniani na kuyataja kuwa ya kihistoria

Baada ya kupita siku kadhaa za mazungumzo hayo huko Geneva hatimaye siku ya Jumapili ya tarehe 24 Novemba kulifikiwa hatua ya kutiwa saini makubaliano ya awali ambayo miradi ya nyuklia ya Iran yenye malengo ya amani ilitambuliwa rasmi na nchi zinazounda kundi la 5+1. Kufuatia kutiwa saini makubaliano hayo, Rais Hassan Rouhani alisema kuwa, taifa la Iran halikuwa na halitakuwa na nia kabisa ya kutengeneza silaha hatari za nyuklia.

 Wakati huo huo Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameisifu timu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inayoshiriki kwenye mazungumzo ya nyuklia na kundi la 5+1 kwa jitihada zake kwenye uwanja huo. Kiongozi Muadhamu ametoa pongezi hizo wakati alipojibu barua aliyoandikiwa na Rais Hassan Rouhani kuhusu mazungumzo hayo.

1322492

captcha