Imam Sayyid Mojtaba Khamenei alitoa ujumbe huo mnamo tarehe 17 Julai, 2026, ukiwaelekea watu watukufu na wapenzi, pamoja na vijana waheshimiwa wa ardhi inayoonewa ya Iraq, kuhusiana na tukio kubwa na tukufu la mazishi ya Kiongozi huyo shahidi mkarimu.
Huu ndio ujumbe huo:
Kwa jina la Mwenyezi Mungu, Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.
Tunatoa salamu, dua, heshima za juu kabisa, na shukrani zetu za dhati kwa Maraji’ (Viongozi wa Kidini) watukufu, wanazuoni waheshimiwa, maprofesa, na wahadhiri wa vyuo vya kidini vya Kiislamu na vyuo vikuu, pamoja na wasomi na viongozi wenye thamani, makamanda, viongozi wa makabila, mashehe, na wakuu wa koo, sambamba na wananchi wema, wenye huruma, na vijana mashujaa na waheshimiwa wa nchi inayoonewa ya Iraq.
Watu wema wa Iraq wamejaliwa fursa adhimu ya kuishi karibu na kuwakaribisha Ahlul-Bayt (amani na rehema za Mwenyezi Mungu ziwashukie wote) katika Haramu zao Tukufu. Wana urithi wa kiutamaduni unaong’aa; wana msingi wa kiroho na mwongozo kama ule wa Chuo cha Kiislamu cha kale na chenye nuru cha Najaf al-Ashraf; na wameonyesha juhudi thabiti katika Mhimili wa Muqawama (Mapambano). Kama watu wa Iran, katika kumpokea Kiongozi shahidi mkarimu (Mwenyezi Mungu ainue daraja yake tukufu), wameunda tukio kubwa la kihistoria lenye maana kuu, lililojawa na huzuni kubwa na ibada ya dhati ya moyoni.
Iraq ilikuwa ardhi iliyobarikiwa tangu wakati nyayo takatifu za Bwana wetu, Amiri wa Waumini [Imam Ali (AS)], zilipogusa udongo wake. Muda mfupi baada ya hapo, watu wake walijipamba kwa fahari kwa vazi la mapenzi na Wilayah kwa Imam Ali na kizazi chake kitukufu (amani na rehema za Mwenyezi Mungu ziwashukie wote).
Vipindi vya utawala wa madhalimu na watawala katili katika ardhi hii havikuweza kamwe kufuta kiini safi cha Wilayah hii na mapenzi kwa Kizazi Kitukufu (cha Mtume) kutoka nyoyoni mwa watu wake. Kwa sababu hii hasa, baada ya kuanguka kwa utawala wa Ba’ath, tukio kubwa la Matembezi ya Arbaeen limeibuka. Kwa vile lilichipuka kutoka vilindi vya nyoyo za watu waaminifu, limezidi kuenea kila uchao.
Na kwa sababu hii hasa, wakati watu hawa waliposhuhudia mwana shahidi anayeonewa [akimuashiria Shahidi Khamenei], mwana wa Imam Ali (AS) na Bwana wa Mashahidi (Imam Hussein AS), ambaye, baada ya miaka ya kutenganishwa kimwili na Haramu Tukufu, sasa alikuwa akirejea kuzunguka maeneo matakatifu yenye nuru katika mwili unaofanana na miili ya mashahidi wa Imam Hussein, mama yake, na ndugu yake, walihirimia kuwasili kwake kwa kila sehemu ya nafsi zao.
Aidha, misafara hii ya mazishi ya mamilioni ya watu kwa ajili ya mbeba bendera wa Muqawama, yamedhihirisha wazi upana kamili wa huruma, udugu, na mshikamano uliopo kati ya mataifa mawili ya Iraq na Iran. Bila shaka, vinara wa Uistikbari wa Kimataifa (Global Arrogance) walishuhudia matukio ya kuvutia ya mkusanyiko huu mkubwa nchini Iraq kwa hofu, wakiona jinsi rasilimali nyingi walizowekeza ili kudhoofisha uhusiano kati ya mataifa haya mawili zimegonga mwamba na kukosa ufanisi.
Kujitokeza huku kwa makumi ya mamilioni ya watu nchini Iran na Iraq kwa ajili ya mazishi na shughuli za kumuaga mujahid Imam shahidi (Mwenyezi Mungu ainue daraja yake tukufu), kumefungua sura mpya ya mwamko na ushirikiano hai wenye lengo la kubadilisha mlinganyo ulioundwa na Mabeberu. Shetani Mkuu, Marekani katili, sasa ametambua kuwa kuendelea kwa uwepo wake wa kibabe na wenye kuleta shida katika eneo hili si kitu kingine isipokuwa ndoto ya kufikirika.
Hivi karibuni, mikono iliyo wazi ya taifa karimu la Iraq, ikiwemo makabila yake karimu na jamii zake, itawakaribisha tena mazuwar wenye shauku wa Arbaeen, wakiwemo umati mkubwa watakaofanya hija hiyo kwa niaba ya Kiongozi shahidi wa Iran. Hii itaingiliana na kumbukumbu ya mazishi yake ya kihistoria na kumbukumbu ya mtu huyo mkuu ambaye labda alikuwa amehifadhi moyoni mwake kwa miaka mingi hamu kubwa ya kuzuru Haramu Tukufu.
Kwa njia hii, kaulimbiu ya kweli kabisa, “Hubb al-Hussein yajma’una” [Mapenzi kwa Hussein yanatuunganisha] itaonyeshwa mbele ya ulimwengu. Na Mwenyezi Mungu akipenda, hii itabarikiwa kwa dua za Bwana wetu (Imam Mahdi), Mwenyezi Mungu aharakishe kudhihiri kwake, kwa ajili ya usalama, baraka, na maendeleo ya taifa la Iraq, kwa njia ya neema na ukarimu wa Mwenyezi Mungu.
Sayyid Mojtaba Hosseini Khamenei
Safar al-Muzaffar 2, 1448 Hijria
26 Tir, 1405 Hijria Shamsia
[17 Julai, 2026]