IQNA

Usomaji wa kipekee wa Qur’ani katika Msimu wa Pili wa Shindano la “Dawlet El-Tilawa” nchini Misri

16:55 - July 18, 2026
Habari ID: 3482503
IQNA – Msururu wa usomaji wa Qur’ani wenye kuvutia ambao uliwapagawisha majaji na hadhira kwa pamoja umeshuhudiwa katika raundi za awali za msimu wa pili wa shindano la “Dawlet El-Tilawa” (Dola ya Usomaji) nchini Misri. Tukio hili linadhihirisha kipaji cha kipekee na juhudi za hali ya juu za washiriki kutoka sehemu mbalimbali za nchi hiyo katika kulihudumia Kitabu Kitukufu.

Miongoni mwa washiriki waliojitokeza kwa umahiri mkubwa ni Mohamed Ahmed Mahfouz Mohamed, kijana mwenye ulemavu wa macho kutoka Mkoa wa Dakahlia, ambaye usomaji wake wa kusisimua uliwaacha majaji katika hali ya mshangao na heshima. Sauti yake yenye nguvu na wakati huo huo yenye kutuliza, Tajwidi yake kamilifu, na utendaji wake wa kutoka moyoni, ulijaza ukumbi mzima na utulivu. Hali hii ilionyesha umahiri wake mkubwa katika usomaji wa Qur’ani na uhusiano wake wa kina wa kiroho na aya hizo tukufu.

Wakati mwingine wa kukumbukwa ulitokana na mtoto Nour El Din Samy El Ghanem kutoka Mkoa wa Damietta, ambaye aliwavutia watazamaji kwa usomaji wake wa kugusa nyoyo na uliowasilishwa kwa urembo wa hali ya juu. Sauti yake ya kuvutia, Tajwidi sahihi, na utendaji wake wa dhati uliunda anga ya utulivu, na kumfanya ajipatie sifa kwa kipaji chake, juhudi, na heshima yake kuu kwa Qur’ani Tukufu.

Katika raundi zote za awali, washiriki walitoa maonyesho ya kusisimua yaliyojaa usahihi, neema, na ikhlasi. Usomaji wao ulibadilisha jukwaa kuwa mahali pa amani na tafakuri, ikionyesha uzuri wa usomaji wa Qur’ani (Qira’a) huku ikisherehekea kizazi kipya cha Maqari wenye vipaji vya hali ya juu ambao wanaendeleza vyema urithi wa Kiislamu katika sanaa ya usomaji wa Qur’ani.

3498305

Habari zinazohusiana
captcha