IQNA

Russia yaonyesha wasiwasi kuhusu maonyesho ya picha zinazomvunjia heshima Mtume SAW

16:15 - November 03, 2008
Habari ID: 1704105
Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amesema kuwa ana wasiwasi kuhusu maonyesho ya picha zinazomvunjia heshima Mtume Muhammad SAW na Masahaba zake katika maonyesho ya Goda huko Uholanzi.
Taarifa iliyochapishwa katika tovuti rasmi ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imelaani vikali hatua hiyo na imezitaka taasisi zote za serikali kuzuia hatua kama hizo zinazokwamisha uhusiano baina ya tamaduni mbalimbali.
Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesema kuwa hatua hiyo inafuatia kitendo cha huko nyuma cha kudhalilisha cha kuchora vibonzo vilivyodaiwa kuwa ni vya Mtume Muhammad SAW ambavyo vilivuruga uhusiano wa Magharibi na ulimwengu wa Kiislamu. 314357





captcha