IQNA

Waislamu wa Australia waikosoa serikali kwa kuunga mkono mchezo wa intaneti wa "Mauaji ya Muislamu"

12:07 - November 05, 2008
Habari ID: 1704829
Waislamu wa Australia wameikosoa serikali ya polisi ya nchi hiyo kwa kuunga mkono mchezo wa intaneti uliopewa jina la "Mauaji ya Waislamu."
Mwandishi wa kujitolea wa IQNA ameripoti kuwa mchezo huo unaopatikana bure katika mtandao wa intaneti ambao mchezaji anapaswa kuua idadi kubwa zaidi ya Waislamu kadiri inavyowezekana, umewakasirisha Waislamu wa Australia. Waislamu hao wameituhumu serikali na polisi ya Australia kwamba wameshiriki katika kubuni mchezo huo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Urafiki ya Waislamu wa Australia Qaisar Trade amewasilisha kesi hiyo kwa Mwendesha Mashtaka Mkuu wa serikali. Amesema katika barua ya mashtaka kwamba, tangu mchezo huo uzinduliwe nchini Australia, vitendo vya matusi, kuwavunjia heshima Waislamu, ubaguzi na utumiaji mabavu dhidi ya Waislamu vimekithiri.
Taasisi ya Ramadhan na Jumuiya ya Vijana wa Kiislamu wa Uingereza pia zimetoa wito wa kupigwa marufuku mchezo huo unaokebehi na kuwavunjia heshima Waislamu. 315658

captcha