Mwandishi wa IQNA ameripoti kuwa Msemaji wa Polisi ya Indonesia ameahidi kuchukua hatua kali baada ya malalamiko yaliyotolewa na jumuiya za Kiislamu za nchi hiyo.
Wakati huo huo Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Indonesia amesema wizara yake inafanya jitihada za kufuatilia maudhui hiyo na kuchukua hatua za kisheria dhidi ya wahalifu hao.
Wizara ya Habari ya Mawasiliano ya Indonesia Jumanne iliyopita iliyataja maonyesho ya picha hizo zinazomvunjia hesmima Mtume Muhammad SAW kuwa hayafai na kuzitaka weblogu zote nchini humo kufuta picha hizo.
Msemaji wa wizara hiyo amesema, maonyesho ya picha hizo yamewavunjia heshima Waislamu na wafuasi wa dini zote za Mwenyezi Mungu. 323506