Sheikh Abdul Amir Qublan ambaye alikuwa akizungumzia safari ya Rais Michael Sulaiman wa Lebanon nchini Iran, amesema Iran ni nchi rafiki na jirani na ina uhusiano sawa wa kidini na Waislamu na Wakristo wa Lebanon.
Sheikh Qublan amesema kuwa safari ya Rais wa Lebanon nchini Iran ina maslahi kwa mataifa yote mawili. Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Mashia wa Lebanon amemshauri Rais wa nchi hiyo kufanya kila awezalo katika safari hiyo kutetea maslahi ya Lebanon.
Rais Michael Sulaiman aliwasili nchini Iran Jumatatu ya wiki hii akiongoza ujumbe wa ngazi za juu wa nchi yake kwa lengo la kustawisha uhusiano wa pande mbili na kuchunguza hali ya mambo katika nchi za Lebanon, Palestina na eneo zima la Mashariki ya Kati kwa ujumla. 325583